• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Watu watano wauawa kwenye shambulizi la mabomu Mogadishu  

    (GMT+08:00) 2017-05-09 10:25:54
    Shambulizi la mabomu dhidi mgahawa mmoja huko Mogadishu, Somalia limesababisha vifo vya watu watano, akiwemo kamanda mmoja mwandamizi wa jeshi, na wengine 10 wamejeruhiwa. Idadi ya vifo inaweza kuongezeka kutokana na hali mbaya ya majeruhi.

    Mashuhuda wamesema gari moja lililokuwa na mabomu liligongeshwa kwenye mgahawa huo ulioko karibu na Ofisi ya Uhamiaji, ambao wateja wake wengi ni wafanyabiashara, wabunge na maofisa wa serikali.

    Shambulizi hilo lilitokea saa chache tu baaada ya rais Mohamed Abdullahi Farmajo kutembelea sehemu ya Lower Shabelle inayodhibitiwa na kundi la Al-Shabaab. Kundi hilo limetangaza kuhusika na shambulizi hilo, na kusema liliwalenga maofisa wa jeshi, idara ya uhamiaji na washauri wa serikali.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako