• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Umoja wa Mataifa wasema pendekezo la "Ukanda Mmoja na Njia Moja" ni mfano wa kuigwa

    (GMT+08:00) 2017-05-09 16:59:12
      Mkurugenzi ya ofisi ya ushirikiano wa nchi za Kusini-Kusini katika Umoja wa Mataifa Bw. Jorge Chediek amesema pendekezo la "Ukanda Mmoja na Njia Moja" lililotolewa na China ni mfano wa kuigwa katika ushirikiano wa nchi za Kusini-Kusini.

    Bw. Chediek amesema kongamano la ushirikiano wa kimataifa la Ukanda Mmoja na Njia Moja litakalofanyika tarehe 14 hadi 15 Mei hapa Beijing, lina uhusiano mkubwa na ushirikiano wa nchi za Kusini-Kusini, na litahimiza zaidi ushirikiano huo.

    Pia amesema pendekezo la "Ukanda Mmoja na Njia Moja" lililotolewa mwaka 2013 litasaidia kuongeza ushirikiano kati ya nchi mbalimbali zinazoendelea, kuchangia maendeleo ya uchumi na ujenzi wa miundombinu katika nchi zinazojumuishwa na pendekezo hilo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako