Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Geng Shuang amesema China inazikaribisha nchi mbalimbali kushiriki kwenye pendekezo la "Ukanda Mmoja na Njia Moja" ambalo ni ushirikiano unaofungua mlango na jumuishi, na kuunganisha mikakati ya maendeleo na kushirikiana kwenye mambo mbalimbali.
Mkutano wa kilele wa ushirikiano wa kimataifa wa "Ukanda Mmoja na Njia Moja" utafunguliwa Jumapili wiki hii, na utahudhuriwa na wakuu wa nchi mbalimbali wakiwemo marais wa Argentina, Chile na Uzbekistan.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |