Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limetangaza kuwa tamasha la vyakula la wakimbizi kwa mwaka huu, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya wakimbizi duniani, litafanyika mwezi wa Juni katika miji 13 mikubwa barani Ulaya, ili kuonesha vipaji vya wakimbizi vya kupika na kuwasaidia kujiunga kwenye jamii za kienyeji. Tamasha la kwanza la vyakula la wakimbizi lilifanyika mwaka jana mjini Paris, ambapo zaidi ya watu elfu moja walionja vyakula mbalimbali vilivyoandaliwa na mapishi wakimbizi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |