Mawaziri wa Serikali ya mpya ya Sudan ijumaa waliapa kikatiba kabla ya rais wa nchi hiyo Omar al-Bashir kuanza majukumu yake. Serikali mpya inaundwa na makamu wawili wa rais, wasaidizi wanne wa rais, shirikisho la mawaziri 31 na mawaziri 43 wa jimbo.
Rais al-Bashir ameeleza alipokuwa akihutubia katika sherehe za kuapishwa kuwa, majukumu ya serikali hiyo ni kutimiza ahadi ya kufanya mazungumzo ya kitaifa.
Jumla ya mawaziri 17 katika serikali ya zamani wameendelea na nafasi zao huku wabunge 64 wameteuliwa kutoka vyama vilivyoshiriki kwenye mazungumzo ya kitaifa.
Serikali mpya ilikuwa imepangwa kutangazwa mwezi Februari lakini ilichelewa kwa sababu ya tofauti ndani ya vyama.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |