Rais Xi Jinping wa China amesema, China ingependa kuimarisha ushirikiano na nchi mbalimbali katika kuhimiza uvumbuzi, na kuzindua mpango wa uvumbuzi wa kisayansi wa "Ukanda mmoja na Njia moja", unaohusu mawasiliano ya kisayansi na kiteknolojia, ushirikiano katika ujenzi wa maabara za pamoja na maeneo ya sayansi na teknolojia, na uhamishaji wa teknolojia. Amesema, katika miaka mitano ijayo, China itawaalika wanasayansi vijana 2,500 kuja China kufanya utafiti kwa mudu mfupi, kutoa mafunzo kuhusu teknolojia na usimamizi kwa watu 5,000, na kuzindua maabara 50 za pamoja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |