Akishiriki katika mkondo wa pili wa mfululizo wa mashindano ya Golden League, Rudisha, ambaye anashikilia rekodi ya dunia, alimaliza wa 4 kwa muda wa 1:45:36
Wakenya wenzake walichukua nafasi tatu za mwanzo wakiongozwa na Kipyegon Bett aliyetumia 1:44:70 akifuatiwa na Robert Biwott na Ferguson Rotich.
Rudisha amesema matokeo hayo mabovu ni kwa sababu hajakimbia kwa muda mrefu tangu mwaka jana aliposhinda dhahabu yake ya pili katika michezo ya Olimpiki mjini Rio de Janeiro.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |