• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais Xi Jinping awaandalia tafrija na maonesho ya sanaa wageni wanaohudhuria mkutano wa Baraza la Ukanda mmoja na Njia moja

    (GMT+08:00) 2017-05-15 08:55:10

    Rais Xi Jinping wa China amewaandalia tafrija na maonesho ya sanaa wakuu wa ujumbe wa nchi mbalimbali na wageni wanaohudhuria mkutano wa kilele wa Baraza la "Ukanda mmoja na Njia moja" hapa Beijing.

    Kwenye tafrija rais Xi Jinping amesema, binadamu wanaishi kwenye jamii moja, na wana hatma ya pamoja. Historia ya binadamu inaendelea kupiga hatua mbele katika maingiliano kati ya watu tofauti na tamaduni tofauti.

    Amesisitiza kuwa "Ukanda mmoja na Njia moja" utazisaidia nchi mbalimbali zijenge dunia iwe jumuiya ya hatima ya pamoja yenye amani, ustawi na masikilizano.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako