• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Shambulizi la mtandao wa internet laathiri kompyuta laki 2

    (GMT+08:00) 2017-05-15 09:07:23

    Shambulizi kwenye mtandao wa internet lililotokea ijumaa iliyopita limeathiri zaidi ya kompyuta laki 2 kwenye nchi 150 duniani.

    Mkuu wa Shirika la Europol Bw Rob Wainwright amesema wahanga wengi ni wafanyabiashara ikiwa ni pamoja na mashirika makubwa, na idadi kubwa namna hii ya nchi zilizoshambuliwa haijawahi kutokea.

    Bw. Wainwright amesema kuwa shambulizi hilo lilitokea ijumaa, idadi ya wahanga huenda itaongezeka kufuatia watu wanaorudi kazini jumatatu baada ya mapumziko ya mwisho wa wiki kuripoti.

    Russia na Uingereza ndio zimeathiriwa zaidi na shambulizi hilo, na idara za afya ndio zimekuwa mhanga mkubwa. Hata hivyo Bw. Wainwright amesema Europol inachunguza chanzo cha shambulizi hilo kwa msingi kwamba lilifanywa na wahalifu na sio magaidi. Pia amesema si pesa nyingi zilizoibiwa kwenye shambulizi hilo, lakini nchini Uingereza madaktari, manesi na maofisa wengine walishindwa kuangalia mafaili ya wagonjwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako