Korea Kaskazini imethibitisha kuwa ilifanya jaribio la kombora la masafa marefu aina ya Hwasong-12 mapema jumapili. Shirika la habari la Korea Kaskazini limesema rais Kim Jong Un wa nchi hiyo alishuhudia jaribio hilo, ambalo lengo lake ni kupima uwezo wa kombora hilo lenye uwezo wa kubeba kichwa kikubwa cha nyuklia. Habari zinasema kombora hilo lilifanikiwa kulenga shabaha yake kwenye bahari kuu iliyokuwa umbali wa kilomita 787.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |