Mali walimiliki mpira kwa muda mrefu na kupanga vyema mashambulizi yao, lakini safu ya ulinzi ya Tanzania ilicheza vizuri na kuokoa hatari nyingi ukiacha chache ambazo mabingwa hao watetezi walipoteza wenyewe.
Mchezo wa pili wa Kundi B ulifuatia jioni ya jana kati ya Niger na Angola baada ya mechi za Kundi A kuchezwa jana Uwanja wa Port Gentil jana wenyeji Gabon wakifungwa mabao 5-1 na Guinea huku Ghana wakianza vizuri kwa ushindi wa 4-0 dhidi ya Cameroon.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |