Ofisi ya uratibu wa masuala ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa OCHA imesema watu wapatao milioni 7.6 nchini Yemen wanaishi kwenye maeneo yenye hatari kubwa ya kuambukizwa ugonjwa wa kipindupindu. Ili kukabiliana na hali hiyo, Umoja wa Mataifa umetoa misaada kwa vituo 33 vya matibabu nchini humo, na pia utaanzisha vituo viwili vya dharura huko Aden nd Sana'a, kwa lengo la kusimamia na kushughulikia maji yaliyochafuka. Mlipuko wa kipindupindu ulioanza tarehe 27 Aprili nchini humo umesababisha vifo vya watu 51 katika wiki mbili zilizopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |