Hata hivyo amekanusha taarifa inayodai kuwa ushiriki wa serikali ya Syria kwenye mazungumzo hayo unalenga kufunika operesheni kubwa zaidi ya kijeshi nchini humo, na kusema mazungumzo ya amani ya Geneva si mazungumzo matupu bali ni mchakato muhimu wa kisiasa wa kuleta amani nchini Syria. Na ajenda ya mazungumzo itakuwa ni kuunda serikali ya umoja, kurekebisha katiba, kufanya uchaguzi mkuu mpya na kupambana na ugaidi.
Habari nyingine zinasema China imesaini makubaliano ya kutoa misaada ya kiuchumi, kiufundi na chakula kwa Syria ili kuisaidia kukabiliana na hali ngumu ya sasa, ikiwa ni hatua ya kutekeleza ahadi iliyotoa China kwenye mkutano wa Baraza la Ukanda mmoja na Njia moja uliofungwa jana hapa Beijing.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |