Ushindi huo uliotokana na bao pekee la mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Amissi Joselyn Tambwe unaifanya Yanga ifikishe pointi 68 baada ya kucheza mechi 29 na itahitaji sare tu kwenye mchezo wake wa mwisho dhidi ya Mbao FC kujihakikishia taji la ubingwa.
Lakini hata sasa, Yanga wanaweza kuanza kushangilia ubingwa kutokana na hazina kubwa ya mabao waliyonao, kwani sasa Simba watatakiwa kuifunga Mwadui FC mabao 13-0 ili kuizuia timu ya Jangwani kutwaa taji kwa mara ya tatu la mfululizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |