• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uchumi wa dunia wakadiriwa kukua kwa asilimia 2.7 mwaka huu

    (GMT+08:00) 2017-05-17 09:44:34
    Ripoti ya makadirio ya hali ya uchumi wa dunia kwa mwaka huu iliyotolewa na baraza la uchumi na jamii la Umoja wa Mataifa imesema uchumi wa dunia unakadiriwa kuongezeka kwa asilimia 2.7 na 2.8 mtawalia mwaka huu na mwaka kesho .

    Mkuu wa kituo cha usimamizi wa uchumi wa baraza hilo Bi. Diana Alarcon amesema kwa sasa uchumi unakua kwa kasi tofauti katika kanda tofauti duniani, ambapo mustakbali wa kanda zilizoko nyuma kimaendeleo baso si mzuri, lakini baadhi ya nchi zilizoendelea na nchi zinazojifanyia mageuzi ziko katika mwelekeo mzuri wa ukuaji.

    Ripoti pia inasema kama kukosekana kwa usawa katika mapato hakutaondolewa, asilimia 35 ya watu katika nchi zilizo nyuma kimaendeleo wataangukia katika umaskini mkali ifikapo mwaka 2030.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako