Orodha ya miradi zaidi ya 270 katika sekta za sera, ujenzi wa miundo mbinu, ushirikiano wa biashara, fedha na mawasiliano ya wananchi imetolewa wakati wa mkutano wa siku mbili za Baraza la kimataifa la "Ukanda mmoja, Njia moja" uliomalizika hivi karibuni hapa Beijing.
Katika miaka mitatu iliyopita tangu pendekezo hilo lilipotolewa, utekelezaji wake umeendelea kwa utaratibu, na kupata matokeo yanayofurahiwa na jumuiya ya kimataifa. Kabla na wakati wa mkutano huo, serikali na kampuni za nchi mbalimbali zilihitimisha matokeo yaliyopatikana katika mchakato wa utekelezaji wa pendekezo hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |