Shirika la mpango wa chakula duniani WFP limetahadharisha kuhusu msukosuko mkubwa wa wakimbizi nchini Uganda, na kusema wastani wa wakimbizi elfu mbili wanaingia Uganda kila siku. Msemaji wa Umoja wa Mataifa Bw. Stephane Dujarric amesema hadi sasa Uganda imepokea wakimbizi milioni 1.2, asilimia 74 kati yao wanatoka Sudan Kusini. Ameongeza kuwa WFP inakosa dola milioni 60 za kimarekani kuwasaidia wakimbizi hao kuanzia mwezi Mei hadi Oktoba mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |