Mgomo mkubwa wa 50 wa wafanyakazi umeanza kote nchini Ugiriki, ukipinga hatua mpya za mageuzi zinazopangwa na serikali ya nchi hiyo, ikiwemo kupandisha viwango vya kodi na kupunguza pensheni. Watu elfu 10 walishiriki kwenye maandamano ya jana mjini Athens. Serikali ya Ugiriki imesema hatua hizo zitaisaidia nchi hiyo kuondoa msukosuko na kurejesha ongezeko la uchumi, lakini waandamanaji wanaona watu wa nchi hiyo hawawezi kuvumilia hasara kubwa zaidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |