• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Umoja wa Ulaya waitaka Uingereza ishirikiane na umoja huo

    (GMT+08:00) 2017-05-18 09:33:40
    Mjumbe wa Umoja wa Ulaya anayeshughulikia masuala ya kujitoa kwa Uingereza Bw. Michel Barnier, amesema Umoja wa Ulaya hauna nia ya kuleta matatizo kwa Uingereza au kuiadhibu kwenye mchakato wake wa kujitoa Umoja wa Ulaya.

    Bw Barnier amemtaka waziri mkuu wa Uingereza Bibi Theresa May kuendelea kushirikiana na Umoja wa Ulaya wakati pande hizo zinafanya mazungumzo badala ya kupingana na kutarajia kufikia makubaliano na Uingereza.

    Bibi Theresa May aliuandikia barua Umoja wa Ulaya mwezi wa Machi na kuanzisha rasmi mchakato wa Uingereza kujitoa umoja wa Ulaya, mchakato ambao utamalizika mwezi wa Machi mwaka kesho. Mazungumzo husika yataanzishwa baada ya uchaguzi mkuu wa nchi hiyo utakayofanyika tarehe 8 mwezi ujao.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako