v CPC waandaa maonyesho ya mafanikio ya awamu ya kwanza ya Rais Xi ikiwemo kuimarika ushirikiano na nchi za Afrika.
WAKATI mkutano wa taifa ya 19 wa Chama cha Kikomunisti (CPC) ukiendelea mjini hapa ,Chama hicho kimefungua maonyesho katika ukumbi mkubwa wa vyumba 10 na kuonyesha mafanikio ya awamu ya kwanza ya utawala wa Rais wa nchi hiyo Xi Jinping ikiwemo mahusiano yaliyopo baadhi ya nchi mbalimbali duniani.
|
v Wakazi wa Beijing wafanya juhudi ya kuhifadhi mfereji mkubwa Mfereji wa kaskazini mjini Beijing ni sehemu ya kaskazini ya mfereji mkubwa wa Jinghang unaojulikana duniani. Mfereji mkubwa wa Jinghang ni mfereji uliochimbwa na watu wenye urefu mkubwa zaidi na historia ndefu zaidi duniani, ukiwa na urefu wa kilomita 1794. Mfereji huo umeunganisha mito mitano kutoka upande wa kaskazini hadi kusini, ukiwemo mto Hai, mto Manjano, mto Huai, mto Changjiang na mto Qiantangjiang. Mfereji huo umeshuhudia busara ya wachina kuishi kwa amani na mazingira ya asili katika enzi ya kilimo na kutuachia urithi wa hazina ya utamaduni. Wakazi wa Beijing wamefanya juhudi ya kuhifadhi mfereji huo.
|
v Maisha mazuri ya mlinzi wa mazingira ya asili wa eneo la chanzo cha mito mitatu nchini China Bw. Zhaxi Cairen mwenye umri wa miaka 28 ni mfugaji aliyezaliwa na kukua katika eneo la ufugaji la mto wa Tuotuo ambao ni chanzo cha mto wa Changjiang. Mwezi wa Agosti, yeye na walinzi wengine wawili wa mazingira ya asili wamebeba mahitaji ya kila siku ikiwemo hema na chakula kuendesha gari kwa umbali wa kilomita 500 kurudi katika kando ya mto wa Tuotuo, ili kufanya doria katika mbuga yenye baridi ambayo ufugaji umepigwa marufuku katika miaka zaidi ya kumi iliyopita.
|
|