Katika mchezo huo ambao Real Madrid ilichomoza na ushindi wa magoli 4 kwa 1 dhidi ya klabu ya Celta Vigo, mchezaji huyo alitupia goli moja kati ya hayo, sasa Madrid inahitaji sare yoyote katika mchezo wake wa mwisho wa ligi wakatapo kutana na klabu ya Malaga jumapili hii, ili kujitangazia Ubingwa wa Ligi. Mahasimu wao klabu ya Barcelona watalazimika kushinda katika mchezo wao wa mwisho wa nyumbani dhidi ya klabu ya Eibar ili kumtia presha zaidi kocha wa Madrid, Zinedine Zidane, na kama mpaka ligi ikimalizika na klabu hizi kulingana alama basi Barca itakabidhiwa kombe, hii ni kutokana na namna Madrid ilivyofungwa zaidi na Barca timu hizi zilipokutana, hivyo Barca itakuwa inachukua ubingwa huu mara ya 3 mfululizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |