Waziri wa mambo ya nje wa Russia Sergei Lavrov ambaye yuko ziarani nchini Cyprus amekanusha madai kuwa rais Donald Trump wa Marekani aliwahi kutoa siri ya kundi la IS kwa Russia.
Bw. Lavrov amesema hayo alipokutana na wenzake wa Cyprus Loannis Kasoulides. Amesema, jambo ambalo rais Trump alisema, ni kwamba kundi la IS limepata njia ya kuficha mabomu yasiyoweza kugunduliwa ndani ya vifaa vya kielektroniki.
Miezi miwili iliyopita Marekani ilipiga marufuku abiria kutoka Asia ya Kati kusafiri kwenda Marekani na kampyuta na vifaa vingine vya kielektroniki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |