Rais Donald Trump wa Marekani ambaye yuko ziarani nchini Saudi Arabia jana amesaini makubaliano pamoja na mfalme Salman wa Saudi Arabia kuhusu biashara ya silaha yenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 110.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu ya Marekani inasema, lengo la kusaini makubaliano hayo ya biashara ya silaha na huduma ni kulinda amani ya Saudi Arabia na kanda ya Ghuba, pia kuongeza uwezo wa Saudi Arabia katika kupambana na ugaidi, ili kupunguza mzigo wa jeshi la Marekani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |