Uswisi imepiga kura za maoni na kupitisha kwa kupata asilimia 58.2 ya kura mswada mpya wa sheria ya nishati uitwao Mkakati wa Nishati 2050. Mswada huo utakaoanza kutekelezwa mwaka kesho unaamua kuwa Uswisi haitajenga vituo vipya vya umeme wa nyuklia, na kuacha kabisa matumizi ya nishati ya nyuklia katika siku zijazo. Mswada huo pia umethibitisha vipaumbele vya kuendeleza nishati endelevu na kuhimiza mageuzi ya nishati.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |