Ligi kuu ya Uingereza (EPL) jana imefika tamati ya msimu kwa mabingwa Chelsea kukabidhiwa kombe lao la ubingwa walioutwaa tangu wiki iliyopita.
Huko Stamford Bridge, Chelsea waliibamiza Sunderland goli 5-1, na baada ya kipenga cha mwisho cha refarii Chelsea na mashabiki wao ilikuwa nderemo kwa kulipokea kombe. Nao Tottenham wameshika nafasi ya 2 kwa kuibamiza Hull City 7-1. Manchester City wakiifunga Watford 5-0 huku Liverpool wakiichapa Middlesbrough 3-0. Kwa hali hiyo Arsenal imeshikilia nafasi ya 5 licha ya kuifunga Everton 3-1 na kuikosa UEFA Champions Ligi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |