Bekia Simba SC, Mohamed Hussein 'Tshabalala' amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa ligi kuu ya Vodacom Tanzaniua Bara wa mwezi Mei kwa msimu wa 2016/2017.
Hussein aliwashinda wachezaji Haruna Niyonzima wa Yanga na Shabani Idd wa Azam FC.
Katika mwezi Mei kulikuwa na raundi 3 ambazo Hussein alicheza kwa dakika zote 270 na kutoa mchango mkubwa katika kuisadia timu yake kubaki katika nafasi ya 2 kwenye msimamo wa ligi kuu ya Vodacom.
Pia alionesha nidhamu ya hali ya juu, hivyo kutopewa onyo la aina yoyote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |