Mabingwa watetezi Mali na timu ya Niger kutoka kundi B, zimefanikiwa kuingia nusu fainali kuungana na Ghana na Guinea kutoka kundi A. Mali iliifumua Angola goli 6-1 na kutwaa ushindi wa kundi A ikiwa na pointi 7 wakati Niger na Serengeti Boys ya Tanzania zikiwa na point 4 kila mmoja lakini Niger inasonga mbele kutokana na rekodi bora dhidi ya Serengeti Boys.
Timu 4 zitakazocheza nusu fainali ndizo zitakazofuzu kucheza fainali za FIFA kombe la dunia kwa vijana chini ya miaka 17 nchini India mwezi Oktoba mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |