Kampuni ya mawasiliano ya Safaricom imefungua kituo cha 45 cha huduma zake nchini Kenya .
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo Bob Collymore amesema hii ni kutokana ongezeko la idadi ya wateja katika eneo la Machakos,Makueni na Kajiado.
Kwa mujibu wa afisa mkuu wa uhusiano mwema wa kampuni hiyo,vituo hivyo husaidia kutoa ajira miongoni mwa wakenya pamoja na kufikisha huduma kwa wateja kwa njia rahisi.
Mwezi uliopita huduma ya kampuni ya Safaricom ilikumbwa na utata kwa zaidi ya saa zita kutokana na hitilafu za mitambo jambo ambalo huenda limesababishwa na idadi kubwa ya wateja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |