Mahakama ya kijeshi nchini jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, imetangaza kukomesha uchunguzi uliokuwa ukifanyika kuhusiana na mauaji ya watalaamu wawili wa umoja wa mataifa waliouawa mwezi Machi huko Kasai ya kati. Mahakama hiyo imesema tayari wanafahamu ni nani aliyehusika na mauaji hayo, baada ya mmoja wa watuhumiwa aliyekamatwa kukiri na kuwataja wenzake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |