Bw. Tedros Adhanom kutoka Ethiopia amechaguliwa kuwa mkurugenzi mkuu wa Shirika la afya duniani WHO. Bw. Adhanom mwenye umri wa miaka 52, ambaye aliwahi kuwa waziri wa afya na waziri wa mambo ya nje wa Ethiopia, alichaguliwa kwenye mkutano mkuu wa 70 wa WHO unaoendelea mjini Geneva, kwa kuchukua nafasi ya Bibi Margaret Chan aliyeongoza shirika hilo kuanzia mwaka 2007. Bw. Adhnom ataanza rasmi muhula wake wa miaka mitano kuanzia Julai 1.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |