Ushindi wa Mali kwa kiasi kikubwa umechangiwa na golikipa wao Youssouf Koita ambaye amefanikiwa kucheza penati tatu za Guinea wakati moja ikitoka nje, ushindi huo sasa unaifanya Mali kucheza mchezo wa fainali dhidi ya timu ya taifa ya Ghana May 28 wakati Guinea itacheza na Niger kutafuta mshindi wa tatu.
Ghana nayo imetinga fainali baada ya kupata ushindi wa penati 6-5 dhidi ya Niger baada ya kwenda sare katika dakika tisini za mchezo.
Na kikosi cha Serengeti Boys kimerejea Tanzania jana kikitokea Gabon na kupokelewa na Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe. Dk Mwakyembe amewapongeza kutokana na walipofikia licha ya kwamba wameshindwa kutimiza ndoto ya kucheza Kombe la Dunia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |