Shirika la ndege la Rwanda Rwandair linazindua safari za moja kwa moja kwenda mjini London Uingereza kuanzia kesho.
Ikiwa hii ndio safari yake ya kwanza kwenda bara Ulaya shirika hilo litatumia ndege yake mpya aina ya Airbus A330.
Itafanya ziara mara tatu kwa wiki ikitua kwenye uwanja wa Gatwick.
Wauzaji wa bidhaa nchini Uigereza wanasema kuanzisha kwa ziara hizo kutawasaidia kwenye biashara zao na pia wasafiri watapata huduma kwa bei nafuu.
Kufuatia ziara hiyo mpya sasa shirika hilo linafikisha 22 maeneo linakohudumu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |