Shirika la ndege la Kenya Kenya Airways imepunguza hasara yake kwa asilimia 60 kwa kupata hasara ya dola milioni 100 katika kipindi kinachokamilika mwezi machi 2017.
Awali shirika hilo lilikuwa na hasara ya dola milioni 560.
Mkurungezi mkuu wa shirika hilo Mbuvi Ngunze amesema licha ya kupungua kwa abiria kumekuwa na ongezeko la kutoka asilimia 4.5 hadi 5.4 .
Hata hivyo ubebaji wa mizigo wa shirika hilo ulipungua kwa asilimia 14.6.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |