• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Michuano ya kombe la dunia chini ya miaka 20 yaendelea kushika kasi Korea Kusini

    (GMT+08:00) 2017-05-26 09:15:30

    Michuano ya kombe la dunia ya vijana chini ya umri wa miaka 20 inaendelea kushika kasi huko nchini Korea ya kusini ikiwa katika ngazi ya makundi.

    Katika michezo ya kundi C wawakilishi wa Afrika timu ya Zambia walipata ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya timu ya Iran. Nao Costa Rica wakatoshana nguvu na Ureno kwa Sare ya bao 1-1.

    Kwenye kundi D Afrika ya kusini walichapwa na Italia kwa mabao 2-0, huku Uruguay wakiwafunga Japani kwa 2-0.

    Michuano hiyo iliendelea tena jana katika kundi E ambapo Ufaransa ikajipatia nafasi ya kucheza hatua ya mtoano baada ya kuibanjua Vietnam kwa magoli 4-0 na kuwafanya wawe vinara wa kundi lao, nao New Zealand baada ya kupepetana na Honduras wakaondoka na ushindi wa 3-1.

    Katika kundi F Saudi Arabia wakapata ushindi wao wa kwanza baada ya kuwagaragaza Ecuador kwa 2-1. Nayo Marekani ikaongoza kundi baada ya kupambana na Senegal na kupata ushindi mwembamba wa goli 1-0.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako