Rais Xi Jinping wa China tarehe 27 mwezi Mei alitoa salamu za pole kwa rais Abdel Fattah el-Sisi wa Misri na jamii ambao ndugu zao wamepoteza maisha na majeruhi katika shambulizi la kigaidi mkoani El Minya nchini Misri.
Rais Xi alisema kuwa, China inapinga aina zote za ugaidi na kulaani vikali shambulizi hilo. China inaunga mkono juhudi za Misri kwa kulinda utulivu na usalama wa taifa na kupinga ugaidi.
Aidha waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang pia alitoa salamu za pole kwa waziri mkuu wa Misri Bw. SherifIsmail.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |