Chama tawala cha Tanzania (CCM) kinatumaini kufahamu na kujifunza uzoefu wa chama cha kikomunisti cha China katika kuongoza kazi ya utoaji wa misaada kwa watu maskini na kupunguza umaskini, na kuhimiza maendeleo ya soko la uchumi.
Hayo yamesemwa na mjumbe wa Kamati kuu ya chama cha mapinduzi cha Tanzania ambaye pia ni naibu katibu wa Ofisi ya Secretariati ya kamati kuu Bw. Pereira Silima ambaye yuko ziarani nchini China.
Ameeleza kuwa, mawazo ya utawala wa chama cha kikomunisti cha China na chama cha Mapinduzi cha Tanzania yanafanana sana na kufuata kanuni za soko la uchumi. Pia amesisitiza kuwa ushirikiano wa kirafiki kati ya vyama hivyo viwili ni msingi muhimu wa siasa kwa pande hizo mbili kuimarisha mawasiliano na ushirikiano na kukuza urafiki.
Bw. Silima ambaye aliongoza ujumbe wa kamati ya utendaji wa taifa wa chama tawala cha nchi hiyo kufanya ziara nchini China.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |