Fainali hiyo iliyokuwa na ushindani wa hali ya juu, timu zote mbili zimepata mabao katika muda wa nyongeza baada ya dakika 90 kumalizika pasipo kufungana.
Mabao ya Simba yamefungwa na Fredrick Blagnon na Shiza Kichuya, bao la kufutia machozi la Mbao FC limefungwa na Robert Ndaki. Kwa ushindi huo Simba imakata tiketi ya kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika kwa mara ya kwanza tangu msimu wa mwaka 2012/13.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |