Bethwel Biwott Yegon amebeba taji kwa upande wa wanaume baada ya kukimbia kwa saa 2:24:00, huku Cheboi Consolata Jepkosgei akinyakua la wanawake kwa kutumia muda wa saa 2:54:15.
Kwa mujibu wa wandaaji, mbio hizo zilijumuisha marathon, nusu marathon marathon ndogo, na kushirikisha wakimbiaji 20,000 kutoka nchi na kanda 41, ikiwemo Kenya, Marekani, Ufaransa, Denmark na Albania.
Wakimbiaji wa kiume kutoka Kenya wamezoa nafasi tatu za juu huku Lu Chunyang na Mei Ying, kutoka China, wakikamata nafasi ya pili na tatu kwa upande wa wanawake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |