• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Reli ya SGR ya Mombasa-Nairobi yaonyesha kasi ya China, ubora wa bidhaa za China, mipangilio mizuri ya China na moyo wa wachina

    (GMT+08:00) 2017-06-01 09:57:01

    Naibu waziri wa mambo ya nje wa China Bw. Zhang Ming amesema, ujenzi wa reli ya SGR ya Mombasa-Nairobi uliopangwa kufanyika kwa miaka mitano, umekamilika kwa miaka miwili na nusu tu, na kuonyesha kasi ya China, ubora wa bidhaa za China, mipangilio mizuri ya China na moyo wa wachina.

    Bw. Zhang Ming amesema anatumai China na Kenya zitashikilia wazo la kutimiza maendeleo kupitia kuinua tija na ufanisi, kuimarisha ujenzi wa maeneo ya viwanda yaliyoko karibu na reli hiyo, na kuhakikisha reli ya SGR na sehemu za karibu na reli hiyo zinatimiza maendeleo endelevu. Pia amehimiza kujenga muundo mpya wa ushirikiano unaojumuisha reli ya Mombasa-Nairobi, bandari ya Mombasa na eneo maalumu la kiuchumi la Mombasa, na kuvifanya kuwa mfano mpya wa kuigwa wa ushirikiano wa kiviwanda kati ya China na Afrika na kunufaisha kihalisi watu wa China na Afrika.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako