Msimu wa ligi ya kikapu ya Taifa nchini Uganda imeendelea kwa kuzikutanisha timu ya Warriors na Reckless Cannons huku Warriors wakiibuka na ushindi wa magoli 65-60.
Kocha wa Canons Nicholas Ntuhereza amekiri kuwa wachezaji wa nyuma wa timu yake hawakucheza vizuri kuwakaba wafungaji na kuruhusu kupoteza mchezo huo.
Canons sasa wamepoteza mechi mbili mfululizo na kushinda mechi moja. Kwa upande wa wanawake, timu ya Lady Canons yenyewe imeibuka na ushindi wa vikapu 56 kwa 27 dhidi ya Lioness.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |