Simba Sports Club ya Tanzania imeaga mashindano ya Sportpesa Super Cup jana baada ya kukubali kipigo cha 5-4 kwa mikwaju ya penalti dhidi ya Nakuru All Stars ya Kenya.
Timu hizi hadi dakika ya 90 zilienda srae ya bila kufungana. Ililazimika kupiga matuta yaamue nani mshindi. Nayo Jang'ombe ya Zanzibar imendolewa baada ya kuadhibiwa na Gor Mahia ya Kenya kwa goli 2-0. Timu pekee ya Tanzania iliyosalia kwenye mashindano hayo ni Dar es salaam Young African ambayo imefanikiwa kufuzu hatua ya nusu fainali huku Kenya zikifanikiwa timu 3 kuingia katika hatua ya nusu fainali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |