Mrusha mkuki Julius Yego wa Kenya amesema sasa analenga kuboresha matokeo yake kwenye mkondo wa nne wa Diamond League msimu huu, Alhamisi ya juma hili atakaposafiri hadi Rome, Italia kushiriki.
Yego alianza msimu kwa kushiriki mkondo wa kwanza wa ligi hiyo, yaliyofanyika Doha Qatar na kupata matokeo yasiyoridhisha akirusha mkuki wake kwa umbali wa mita 81.94 iliyomwacha katika nafasi ya 7 katika jedwali la urushaji mkuki linaloongozwa na Mjerumani Rohler Thomas aliyerusha umbali wa mita 93:90.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |