Safari ya kutinga fainali za kombe la Dunia la 2018 huko Russia inaendelea Ijumaa Juni 9 kwa nchi za Ulaya na miongoni mwa mechi zake ni mitanange kati ya Sweden na France na ule wa watani wa Jadi Scotland na England. Mechi zingine zitazikutanisha timu za Bosnia and Herzegovina watakutana na Greece (kundi H), Uholanzi watamenyana na Luxembourg (kundi A), Belarus wataumana na Bulgaria (kundi A) Portugal na Latvia (kundi B), Faroe Island watakutana na Switzerland (kundi B), huku Estonia wataumana na Belgium (kundi H), nao Andorra watakutana na Hungary (kundi B) na Gibraltar itakutana na Cyprus (kundi H)
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |