Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao, amesema hisa hizo zitakuwa za kihistoria na zitavunja rekodi kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam kwa miaka 19 tangu kuanzishwa kwake.
Hii imechangia kwa kiasi kikubwa malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kutaka kuona Watanzania wanakuwa wamiliki wa kampuni kubwa zinazofanya biashara nchini.
Katika taarifa yake, Ferrao amesema, Vodacom Tanzania PLC inajivunia kuwa kampuni ya mawasiliano inayoongoza Tanzania na ndiyo kampuni ya kwanza kutimiza masharti ya Bunge la Tanzania ya kutaka makampuni zote za simu za mkononi kuorodhesha hisa zake kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |