Ni mara ya pili kwa shirika hilo kushinda tuzo hilo linalotolewa kwenye maonyesho ya usafiri wa anga.
Mwaka huu maonyesho hayo yamefanyika mjini Johannesburg Afrika Kusini.
Shirika hilo limetambuliwa kwa juhudi zake za upanuzi, kupanda kwa faida na kuchangia ukuaji wa sekta ya usafiri wa anga barani Afrika.
Licha ya kuwa na kipindi kigumu kwenye sekta hiyo mwaka hu, mkurungezi wa shirika hilo Meseret Bitew, amesema wamefanikiwa kuboresha huduma na pia kuongezea maeneo zinakosafiri ndege zake.
Faida ya mwaka 2016 ya shirika hilo imekua kwa asilimia 70 ambako ilipata dola milioni 265 huku wasafiri wakiongezeka kwa asilimia 18.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |