• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania yatangaza bajeti yake

    (GMT+08:00) 2017-06-09 19:16:13
    Bajeti ya Tanzania kwa mara ya pili imeendelea kugusa maisha ya wananchi wa kawaida wa Tanzania baada ya kutangaza hatua kadhaa zilizojielekeza kuwaondolea mzigo na kuwafanya wawe na maisha bora.

    Akitangaza bajeti ya mwaka wa 2017/2018, waziri wa fedha wa Tanzania Dk Philip Mpango amesema walifikia hatua hiyo baada ya kuridhishwa na hatua zilizochukuliwa na serikali ambazo zimeonekana dhahiri zitawaondolea mzigo wananchi wa Tanzania. Miongoni mwa mambo mazuri ya bajeti hiyo ni kufuta ada ya kila mwaka ya leseni ya magari; kufuta ada ya ukaguzi wa viwango vya mazao ya biashara; kutoza kodi ya VAT kwa kiwango cha sifuri kwa huduma zinazotolewa kwenye usafirishaji wa bidhaa/mizigo nje ya nchi.

    Pia serikali imetangaza kuwatambua rasmi wafanyabiashara ndogo wasio rasmi kama machinga, mama lishe, wauza mitumba, kutoza ushuru wa forodha kwa kiwango cha asilimia 0 badala ya asilimia 25 kwenye malighafi na vifaa vinavyoagizwa nje kwa ajili ya kuunganisha na kutengeneza vifaa ambavyo ni mahsusi kwa ajili ya matumizi ya walemavu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako