Serikali ya Tanzania ili tia saini mkataba wa dola milioni 154 siku ya Jumamosi na kampuni ya China ya Bandari (Chec) ili kupanua bandari kuu katika mji mkuu wa biashara, Dar es Salaam.
Tanzania inatafuta fedha kwa ajili ya miradi ya miundombinu kama sehemu ya mipango yake ya kubadili nchi kuwa, kitovu cha usafiri na biashara.
Upanuzi wa bandari nchini Tanzania, inatarajiwa kuongeza ushindani kwa watumiaji bandari.
Tanzania chini ya mkataba unafadhiliwa na benki ya Dunia ya mkopo, CHEC, kampuni tanzu ya serikali inayoendeshwa na kampuni ya mawasiliano na ujenzi ya China, itajenga kituo ambacho kitaimarisha mahali pa meli kutia nanga katika bandari ya Dar es Salaam.
Tanzania inatarajia upanuzi wa bandari utaongeza chombo cha mizigo hadi tani milioni 28 ifikapo mwaka 2020 kutoka tani milioni 20 iliyo sasa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |