Benki Kuu imeshauri serikali ya Uganda kuwacha kuchukua mikopo kwani deni la sasa nchini ni kubwa.
Madeni ya nje na ndani nchini Uganda imefikia dola bilioni 8.7.
Kulingana na Adam Mugume mkurungenzi mkuu wa utafiti katika Benki ya Uganda, ni kwamba katika miaka miwili iliyopita imekuwa ikikopa kwa kiwango cha asilimia 17 kila mwaka kutoka hazina ya malipo ya uzeeni (NSSF).
Mugume amekaribisha uamuzi wa serikali kupunguza mikopo ya ndani huku akisema itatengeneza rasilimali zaidi kwa ajili ya benki za biashara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |