Muingereza Lewis Hamiliton kutoka Mercedes alimpoteza Sebastian Vettel wa Ferrari ambaye anatajwa kama mpizani wake mkubwa baada ya Hamilton kuibuka kidedea katika michuano hiyo huku akimuacha mbali Sebastian Vettel ambaye aliishia kushika nafasi ya 4 katika mbio hizo.
Nafasi ya 2 ilishikwa na dereva mwenzake kutoka Mercedes, Valtteri Bottas huku nafasi ya 3 ikishikiliwa na Daniel Ricciardo toka Redbull. pamoja na Hamilton kushinda mashindano hayo ila Sebastian Vettel bado anaongoza msimamo wa madereva wa Formula One huku Lewis Hamilton akiwa katika nafasi ya pili,
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |