Rais Xi Jinping wa China amesema kuwa China inategemea Luxembourg itachukua nafasi muhimu katika kuendeleza uhusiano kati ya China na Umoja wa Ulaya.
Rais Xi amesema hayo alipokutana na waziri mkuu wa Luxembourg Xavier Bettel ambaye yuko ziarani hapa China. Rais Xi amesema kuwa anatumaini kuwa Luxembourg inaweza kuushawishi Umoja wa Ulaya kutoa masharti nafuu kwa ajili ya maendeleo ya ushirikiano kati ya China na Umoja huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |